Kwa zaidi ya wiki tatu sasa, sukari imeendelea kuumiza vichwa wafanyabiashara na watumiaji kwa upande mmoja na serikali kwa upande mwingine nchini Tanzania.
Huku sokoni na madukani ikiwa imeadimika, kule inakopatikana bei yake haishikiki.
Lakini kiasi kikubwa cha uhitaji wa sukari nchini Tanzania kinaweza kuzalishwa kutoka ndani, kwa nini sasa sakata hili la sukari liendelee kuisakama zaidi?
Mwandishi wetu Sammy Awami, ametuandalia taarifa hii.