Get New DJ Mixes
ENTERTAINMENT

Mdundo Yabadilisha Tasnia ya Mziki kwa Kuwezesha Malipo ya Mirabaha Ya Haki

Mdundo Yabadilisha Tasnia ya Mziki kwa Kuwezesha Malipo ya Mirabaha Ya Haki

Mdundo Yabadilisha Tasnia ya Mziki kwa Kuwezesha Malipo ya Mirabaha Ya Haki

Katika hatua ya kuvunja mipaka ambayo inakusudia kubadilisha mandhari ya muziki barani Afrika, Mdundo, jukwaa kuu la kusikiliza na kupakua muziki barani Afrika, imethibitisha dhamira yake thabiti ya kuunga mkono wasanii na kubadilisha tasnia kupitia mfumo wa malipo ya haki na uwazi. Kwa kutabiri kulipa kiasi kikubwa cha dola milioni 1.2 hadi 1.5 katika kipindi cha miezi 12 ijayo, Mdundo inadhamiria kukuza mafanikio ya kifedha ya wasanii na kuchangia muundo, sheria, na kipato katika sekta ya muziki.

Mdundo inajivunia kikosi chake kikubwa na tofauti cha wanamziki na wenye vipindi zaidi ya 100,000, hivyo kujitengeza kama jukwaa kuu la kugundua muziki barani Afrika. Kwa kushirikiana na lebo mashuhuri kama Africori, MAD, Mavin, Universal Music Group, Warner Music, na nyingine nyingi, Mdundo inahakikisha watumiaji wake 24.5 milioni kila mwezi wanafurahia muziki kutoka muziki wa aina tofauti, mitindo, na mikoa.

Subscribe ili kupata DJ mixes zaidi hapa: https://mdundo.ws/cloudsblog

Moja ya nguzo kuu za malengo ya Mdundo ni kuunga mkono wanamuziki wa Kiafrika na kuhakikisha wanapata mafao yanayowastahili. Hadi sasa, takribani wasanii 156,000 wa Kiafrika wamenufaika na mfumo wa malipo wa kipekee wa Mdundo. Jukwaa hili linafanya hesabu kwa umakini ya mafao ya msanii kwa nchi, kama ifuatavyo:

Kenya: 35% (wasanii 58,000 wanaofanya kazi)
Tanzania: 19% (wasanii 15,000 wanaofanya kazi)
Nigeria: 17% (wasanii 24,000 wanaofanya kazi)
Afrika Kusini: 8% (wasanii 8,000 wanaofanya kazi)
Uganda: 6% (wasanii 21,000 wanaofanya kazi)
Ghana: 6% (wasanii 7,000 wanaofanya kazi)

“Mdundo Artist Royalty Payment ni uthibitisho wa lengo letu la kuwawezesha wasanii na kuchochea ukuaji wa muziki wa Kiafrika,” alisema Wanjiku Koinange, Mkuu wa Muziki wa Mdundo. Kwa kuzingatia fidia ya haki, Mdundo inalenga kukuza mfumo ambapo ubunifu unaweza kuchanua.

“Tunafurahi kuwa sehemu ya safari ya Mdundo na kuona ukuaji mkubwa katika malipo ya haki,” alisema Michael Mlingwa, Afisa Mtendaji Mkuu wa Slide Digital. “Ushirikiano wetu umetuwezesha si tu kifedha bali pia kutimiza ndoto za wasanii na kuwafikia hadhira kwa kiwango kikubwa. Pamoja, tunakifanyia sura ya muziki ya siku zijazo.”

Mdundo inaendelea kuongeza wigo wake barani Afrika na hata zaidi, inakaribisha wasanii na lebo za rekodi zingine kujiunga na kufahamu athari chanya ya jukwaa kwa vitendo. Kwa kujiunga na jamii inayojitokeza ya Mdundo, wasanii wanaweza kufungua fursa mpya za ukuaji, huku wakifurahia faida za malipo ya haki na uwazi.

Kwa wasanii na lebo za rekodi wanaopenda kujifunza zaidi kuhusu Mdundo na Malipo ya Haki ya Wasanii yanayokuja, tembelea https://www.mdundoforartists.com/ au wasiliana na artist@mdundo.com. Mdundo kwa hakika inabadilisha tasnia ya muziki, kuwawezesha wasanii wa Kiafrika, na kubuni mustakabali wa muziki barani.